Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 18 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 154 2021-04-28

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Tingi – Kipatimu yenye urefu wa kilometa 50 kwa kiwango cha lami hasa ikizingatiwa kuwa barabara hiyo inapita katika maeneo yenye kumbukumbu za Vita vya Majimaji na vivutio muhimu vya Utalii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa ujenzi wa barabara ya Tingi – Kipatimu yenye urefu wa kilometa 50 kwa kiwango cha lami. Hata hivyo, mkakati wa Serikali kwa sasa ni kuunganisha makao makuu ya mikoa kwa barabara za lami zilizoainishwa kwenye shoroba za maendeleo (development corridor). Serikali itakapokamilisha mpango huu barabara nyingine za mikoa zitafuata ikiwemo barabara ya Tingi – Kipatimu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na matengenezo ya kawaida na matengenezo ya muda maalum ili kuifanya barabara hii kupitika majira yote ya mwaka ambapo katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya shilingi milioni 496.569 zimetengwa kwa ajili ya kuifanyia matengenezo barabara hii. Aidha, Serikali imepanga kuimarisha baadhi ya sehemu korofi kwa kuziwekea lami. Ahsante.