Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 2 | sitting 3 | Water and Irrigation | Maji na Umwagiliaji | 32 | 2016-01-28 |
Name
Neema William Mgaya
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:-
Kumekuwa na tatizo kubwa la upatikanaji wa maji katika Mji wa Makambako:-
Je, Serikali imejipangaje kutatua tatizo hilo?
Name
Eng. Isack Aloyce Kamwelwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Katavi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema William Mgaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kupita awamu ya kwanza ya programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (Water Sector Development Program - WSDP) imekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa mradi wa maji wa Makambako. Kazi zitakazotekelezwa katika mradi huu ni pamoja na ujenzi wa bwawa la Tagamenda, uchimbaji wa visima virefu vya Idofi na chemichemi ya Bwawani, ujenzi wa bomba kuu na mfumo wa usambazaji wa maji na matanki makubwa ya kuhifadhi maji. Mradi huu unakadiriwa kugharimu kiasi cha wastani wa shilingi za Kitanzania bilioni 70.3 sawa na dola za Marekani milioni 32.39 na unatarajiwa kunufaisha wananchi wapatao 155,233.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ujenzi wa Mradi wa Maji Makambako utatekelezwa katika awamu ya pili ya Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP II) katika mwaka wa fedha 2016/2017. Hivi sasa Serikali inakamilisha taratibu za kupata mkopo wa gharama nafuu kutoka Serikali ya India kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo. Katika mwaka wa fedha 2015/2016, Serikali ilitenga shilingi bilioni moja ili kuboresha hali ya huduma ya maji katika Mji wa Makambako. Wakati mradi mkubwa unasubiriwa na pindi fedha zikipatikana kabla ya mwaka kumalizika fedha hizo zitatumwa.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved