Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 17 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 144 2021-04-27

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza:-

Je, ni gharama kiasi gani na taratibu gani hutumika ili kupata huduma za ulinzi za SUMA JKT?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, huduma ya Ulinzi toka SUMA JKT Guard inapatikana kupitia njia kuu nne, ikiwemo:-

(1) Idara ya masoko kutembelea wadau wa huduma ili kutangaza shughuli za kampuni;

(2) Mteja mwenyewe kuwasilisha barua za maombi ya kupatiwa huduma ya ulinzi;

(3) Kampuni imesajiliwa katika mfumo wa manunuzi ya Serikali ya TANEPS ambapo wadau, hasa Taasisi za Serikali hutumia kutangaza zabuni.

(4) Ushiriki katika mchakato wa zabuni shindanishi zinazotangazwa kupitia magazeti na vyombo vya habari.

Mheshimiwa Spika, naomba nifafanue zaidi kuwa gharama ya kupata huduma za ulinzi za SUMA JKT Guard kwa mlinzi mmoja bila silaha ni shilingi 590,000 kwa mwezi ikijumuisha VAT, lakini silaha moja ni shilingi 129,800 hivyo mlinzi akiwa na silaha, gharama yake ni shilingi 719,800 kwa mwezi. Huduma ya mlinzi mmoja kwa maeneo ya migodini ni shilingi 944,000/= ikiwa ni pamoja na VAT kwa mwezi.