Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 17 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 143 2021-04-27

Name

Augustine Vuma Holle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Vijijini

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA K.n.y. MHE. AUGUSTINE V. HOLLE aliuliza:-

Kumekuwa na mgogoro wa ardhi wa muda mrefu baina ya Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu na Kata ya Makere:-

Je, ni lini Serikali itatatua mgogoro huo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi, naomba sasa kujibu swali la Mheshimiwa Augustine Vuma Holle, Mbunge wa Kasulu Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu ilianzishwa mwaka 1996 kwa ajili ya kupokea wakimbizi kutoka nchi ya DRC. Wakati wa uanzishwaji wa kambi hiyo hakukuwa na mgogoro wa ardhi kwa sababu lilikuwa ni eneo lisilotumika. Aidha, pamoja na eneo la kambi, Serikali ilitenga eneo lingine la kambi kwa ajili ya wakimbizi iwapo eneo la awali litazidiwa.

Mheshimiwa Spika, kadiri ya muda ulivyoenda, wananchi walianza kuvamia eneo la akiba kwa lengo la kuwatumia wakimbizi kama vibarua katika shughuli za kilimo katika eneo hilo. Kwa kuzingatia maelezo hayo, ni wazi kuwa hakuna mgogoro wa ardhi baina ya Kambi ya Nyarugusu na Kata ya Makere, bali ni suala la uelewa ambapo wananchi wanaendelea kuelimishwa juu ya matumizi sahihi ya eneo hilo.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na jitihada za kumaliza tatizo la wakimbizi nchini kwa kuwarejesha wakimbizi makwao kwa kushirikiana na Jumuiya za Kimataifa na nchi wanazotoka wakimbizi hao. Baada ya wakimbizi hao kuondoka maeneo yote ya kambi za wakimbizi yatarejeshwa Serikalini ili mamlaka zinazohusika ziweze kuyapangia matumizi stahiki.

Mheshimiwa Spika, ahsante.