Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 17 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 141 2021-04-27

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA aliuliza:-

Mwaka 2015 wakati wa Kampeni, Mhe. Rais aliahidi kujenga barabara ya kilometa tatu katika Mji wa Kakonko ambao ndiyo Makao Makuu ya Wilaya.

Je, kwa nini ahadi hiyo haijatekelezwa na ni lini sasa itatekelezwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aloyce John Kamamba, Mbunge wa Jimbo la Buyungu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kutekeleza ahadi ya aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa awamu. Katika mwaka wa fedha 2020, Serikali imeanza ujenzi wa barabara yenye urefu wa mita 630 kwa kiwango cha lami katika Mji wa Kakonko itakayogharimu shilingi milioni 500. Ujenzi huu umefikia asilimia 80 na unatarajiwa kukamilika mwezi Mei 2021.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya barababara nchini ikiwemo Wilaya ya Kakonko kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.