Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 16 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 136 2021-04-23

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID Aliuliza:-

Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi huchangia Pato la Taifa kutokana na shughuli za utalii.

Je, Serikali haioni kuwa umefika wakati wa kuukarabati Uwanja wa Ndege wa Same Mjini ili ndege ndogo na za kati ziweze kutua kuleta watalii wa ndani na nje ya nchi katika Hifadhi ya Mkomazi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na ushauri wa Mheshimiwa Dkt. David Mathayo David, Mbunge wa Same Magharibi, kuhusu ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Same, Serikali itaangalia uwezekano wa kukifanyia ukarabati kiwanja hicho kwa kadri ya upatikanaji wa fedha ili kuongeza Pato la Taifa kupitia sekta ya utalii. Ahsante. (Makofi)