Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 14 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 119 2021-04-21

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Chuo cha VETA Shaurimoyo – Ludewa ili kuzalisha Wataalam watakaosaidia kutekeleza mradi wa Liganga na Mchuchuma utakapoanza?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Ludewa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi na Huduma cha Mkoa wa Njombe kinachojengwa katika Wilaya ya Ludewa ni miongoni mwa vyuo vilivyokuwa vinajengwa na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia mradi wa kuimarisha Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi na Elimu ya Ualimu (STVET – TE). Mradi huu ulikuwa unafadhiliwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ambapo mkataba kati ya Serikali na Benki hiyo uliisha muda wake tarehe 31 Desemba, 2019, kabla mradi haujakamilika.

Mheshimiwa Spika, kutokana na umuhimu wa kukamilika kwa mradi huu, utekelezaji wa mradi huu utaendelea kupitia Mradi wa Kukuza Ujuzi na Stadi za Kazi (ESPJ) kwa utaratibu wa “Force account”. Tathmini ya gharama imeshafanyika ambapo jumla ya shilingi 4,342,678,784.32 zitatumika katika kukamilisha ujenzi huu. Ujenzi wa Chuo hiki unatarajiwa kuanza tena katika Mwaka wa Fedha 2020/2021. Ahsante.