Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 14 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 118 2021-04-21

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA J. MDEE aliuliza:-

(a) Je, ni nini sababu ya kuweka tozo ya ada ya tathmini ya asilimia moja kwa mkopaji wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo ambapo asilimia 50 inalipwa kabla ya kuanza kufanya tathmini na asilimia 50 inalipwa baada ya mkopo kuidhinishwa?

(b) Je, ni kigezo gani kilisababisha tozo kuwa asilimia 1 na si vinginevyo?

(c) Je, mkopo usipoidhinishwa hiyo asilimia 50 ya asilimia moja iliyolipwa inarudishwa ama la?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Halima James Mdee, kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, ada ya tathmini ya mikopo inayotozwa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo ya Tanzania ni kwa ajili ya kulipia gharama za uchambuzi wa maombi ya mkopo ambayo ni pamoja na shajara, uhakiki wa mradi pamoja na dhamana ya mkopo.

(b) Mheshimiwa Spika, kigezo kinachotumika kutoza ada ya uchambuzi wa maombi ya mikopo ni gharama halisi za uchambuzi wa maombi ya mkopo zinazotokana na nguvu ya soko kwa wakati husika. Aidha, utaratibu huu ni wa kawaida kwa taasisi za fedha kutoza ada ya uchambuzi wa maombi ya mikopo.

(c) Mheshimiwa Spika, endapo mkopo hautaidhinishwa, asilimia 50 ya asilimia moja iliyolipwa huwa hairejeshwi kwa mwombaji wa mkopo kwa kuwa kiasi hicho kinakuwa kimetumika kulipia gharama za uchambuzi wa mkopo.