Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 16 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 137 2016-05-10

Name

Muhammed Amour Muhammed

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Bumbwini

Primary Question

MHE. MUHAMMED AMOUR MUHAMMED aliuliza:-
Kumekuwa na unyanyasaji mkubwa unaofanywa na JWTZ wa kuwanyang‟anya wavuvi samaki wao licha ya kwamba watu hao wanajitafutia kipato kupitia bahari kama Watanzania.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuondoa unyanyasaji huo unaofanywa na Jeshi la Wananchi kwa wananchi wake?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Muhammed Amour Muhammed, Mbunge wa Bumbwini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa haijawahi kupokea tuhuma yoyote inayohusu unyanyasaji unaofanywa na askari wa JWTZ kwa wavuvi nchini. Aidha, kama tuhuma hizi zina ushahidi ni bora zikafikishwa sehemu husika ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua zinazostahili.
Mheshimiwa Spika, nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Bunge lako Tukufu kwamba, wanajeshi kama walivyo raia wote wanapaswa kuheshimu sheria za nchi na pale wanapokwenda kinyume huchukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa sheria na kanuni za jeshi.