Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 13 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 106 2021-04-20

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha VETA katika Jimbo la Mbulu Vijijini ili vijana wapate ujuzi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Flatei Gregory Massay, Mbunge wa Mbulu Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na mpango wa kujenga Vyuo vya Ufundi Stadi ikiwa na lengo la kuwa na Chuo cha Ufundi Stadi katika kila mkoa na wilaya. Serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ilitenga jumla ya shilingi bilioni 48.6 kwa ajili ya kujenga vyuo 29 vya VETA katika ngazi ya Wilaya ambavyo kwa sasa vipo katika hatua mbalimbali za ujenzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Wilaya ya Mbulu kuna Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Tango ambacho pia hutoa mafunzo ya ufundi stadi. Chuo hiki kinaendelea na ukarabati na ujenzi wa miundombinu utakaogharimu jumla ya shilingi milioni 605.2 ambao unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo, katika kipindi hiki ambacho Serikali inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha VETA wilayani humo, nashauri wananchi wa Jimbo la Mbulu Vijijini kuendelea kutumia vyuo vilivyopo maeneo yote nchini, ikiwa ni pamoja na Chuo cha Maendeleo ya Wananchi - Tango na Chuo cha VETA Manyara. Ahsante.