Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 12 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 102 2021-04-19

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Primary Question

MHE. BONNAH L. KAMOLI K.n.y. MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia Wananchi wa Chalinze waliopisha ujenzi wa miundombinu ya miradi ya kusafirisha umeme kutoka Kinyerezi na Bwawa la Mwalimu Nyerere?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Kikwete, Mbunge wa Chalinze, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO inatekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovolti 400 kutoka Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Mwalimu Julius Nyerere hadi Chalinze lakini pia ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme katika Kijiji cha Chaua - Chalinze.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia TANESCO imekamilisha tathimini ya mali za wananchi na Taasisi zilizopisha utekelezaji wa mradi huu na fidia kuidhinishwa na Mthamini Mkuu wa Serikali. Jumla ya shilingi bilioni 42.3 zimetengwa katika bajeti ya mwaka 2021/2022 kwa ajili ya malipo ya fidia kwa wananchi waliopisha mradi. Fidia ya wananchi hao itaanza kulipwa muda wowote kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 baada ya taratibu zote kukamilika.