Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 12 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 100 2021-04-19

Name

Hamis Mohamed Mwinjuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Primary Question

MHE. HAMIS M. MWINJUMA aliuliza:-

Kasi ya ujenzi wa barabara ya Muheza – Amani sio ya kuridhisha na hadi sasa maeneo korofi bado hayajafikiwa:-

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuwa na awamu ya pili katika ujenzi wa barabara hiyo kuanzia Amani kuelekea Muheza ili kutatua changamoto zilizopo wakati ujenzi wa barabara ukiendelea?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamis Mohamed Mwinjuma, Mbunge wa Muheza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia umuhimu wa barabara ya Muheza – Amani yenye urefu wa kilometa 40, Serikali iliamua kuijenga kwa kiwango cha lami kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha baada ya kukamilika kwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina mwaka 2015. Awamu ya kwanza ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sasa yenye urefu wa kilometa saba kuanzia Muheza kuelekea Bombani inaendelea na imefikia asilimia 70.

Mheshimiwa Spika, mara baada ya kukamilika kwa sehemu ya kwanza ya mradi huu unaoendelea, ujenzi wa sehemu ya pili ya kuanzia Bombani hadi Amani utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha. Lengo ni kukamilisha ujenzi wa barabara yote kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha za kukamilisha ujenzi wa sehemu ya barabara iliyobaki, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii ikiwemo sehemu korofi ili kuhakikisha inapitika majira yote. Katika mwaka wa fedha 2020/2021, barabara hii ilitengewa shilingi milioni 600 kwa ajili ya matengenezo mbalimbali, ahsante.