Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 12 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 98 2021-04-19

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:-

Je, Serikali haioni haja kukipandisha hadhi Chuo cha Ualimu Nachingwea kuwa Chuo Kikuu cha Ualimu kutokana na mahitaji ya Walimu kuwa makubwa?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tecla Mohamed Ungele, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, lengo la kuanzisha vyuo vya ualimu hapa nchini, kikiwemo Chuo cha Ualimu Nachingwea, ni kuhakikisha kuwepo kwa walimu mahiri na wanaotosheleza mahitaji ya walimu katika ngazi ya elimu ya awali, msingi, sekondari na elimu ya watu wazima. Vilevile, Vyuo hivi vina jukumu kubwa la kuwezesha mafunzo ya walimu kazini ambapo walimu walio karibu na vyuo hivyo hupata nyenzo mbalimbali za kitaalamu ili kuboresha ujifunzaji na ufundishaji shuleni.

Mheshimiwa Spika, ongezeko kubwa la wanafunzi na shule katika ngazi ya elimu ya awali, msingi na sekondari kutokana na Sera ya Elimu Bila Malipo, limesababisha kuwepo kwa uhitaji mkubwa wa walimu katika ngazi hizo. Ili kukidhi mahitaji ya walimu katika ngazi hizo, Serikali inaendelea na ujenzi na ukarabati wa miundombinu mbalimbali ya vyuo vya ualimu, uwekaji wa samani pamoja na vifaa vya kufundishia na kujifunzia. Chuo cha Ualimu Nachingwea ni miongoni mwa vyuo vilivyofanyiwa ukarabati na ujenzi kwa gharama ya shilingi bilioni 1.9.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mahitaji ya walimu, hususan katika ngazi ya elimu ya awali na msingi ni makubwa kutokana na ongezeko kubwa la shule na wanafunzi katika ngazi hiyo, Chuo cha Ualimu Nachingwea bado kinahitajika katika kuandaa walimu wa stashahada na astashahada.

Mheshimiwa Spika, hivyo, wanafunzi wa shahada wanaweza kuendelea kudahiliwa na vyuo vikuu vilivyopo nchini kwa kuwa, bado vina uwezo wa kufanya hivyo. Ahsante.