Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 11 Water and Irrigation Wizara ya Maji 93 2021-04-16

Name

Martha Festo Mariki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTHA F. MARIKI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto ya maji katika Mkoa wa Katavi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Martha Mariki, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji Mkoa wa Katavi ni asilimia 70. Serikali kupitia Mamlaka ya Maji na Usafi wa Mazingira Mpanda inatekeleza miradi miwili ya maji ambayo ipo katika hatua za mwisho za utekelezaji na imeshaanza kutoa huduma ya maji. Kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa banio, ulazaji wa bomba kuu umbali wa kilomita 24 kutoka katika chanzo cha maji Ikolongo II na ujenzi wa tenki la lita milioni moja kwa ujumla wa mradi, unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Aprili, 2021.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea kuboresha huduma ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa Manispaa ya Mpanda ambapo mji huo ni miongoni mwa miji 28 itakayonufanika na utekelezaji wa mradi wa maji kupitia fedha za mkopo kutoka Serikali ya India. Kazi hii inatarajiwa kuanza hivi karibuni na itachukua miezi 24. Aidha kupitia RUWASA utekelezaji wa miradi 30 unaendelea na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2021. Miradi hii, ikikamilika jumla ya vijiji 138 vya Mkoa wa Katavi vitakuwa na huduma ya maji ya uhakika, hivyo kutoa nafasi kwa wananchi kufanya kazi za maendeleo.