Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 11 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 89 2021-04-16

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:-

Je, ni lini utekelezaji wa mradi wa kuendeleza Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW) utaanza?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum Iringa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Kuendeleza Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW) tayari umeanza kutekelezwa tangu mwaka 2017. Mradi huu unatekelezwa kwa mkopo wa Dola za Kimarekani milioni 150 kutoka Benki ya Dunia katika maeneo ya kipaumbele zikiwemo Hifadhi nne za Taifa ambazo ni Hifadhi ya Taifa Ruaha, Mikumi, Nyerere, Milima Udzungwa na maeneo yanayozunguka hifadhi hizo pamoja na eneo la chanzo cha maji cha Mto Great Ruaha. Mradi huu unatekelezwa kwa kipindi cha miaka sita kuanzia mwaka 2017 - 2023.

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwezi Machi 2021, mradi huu umeendelea kutekelezwa kwa ufanisi mkubwa ambapo kazi zifuatazo zimetekelezwa: ununuzi wa vifaa vya doria vimeshanunuliwa, magari 44 yameshanunuliwa, mitambo mikubwa mitatu kati ya 18 inayotarajiwa kununuliwa, pia mradi umeajiri kampuni sita ambazo zinaendelea na usanifu wa majengo, barabara na viwanja vya ndege.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, kutokana na changamoto mbalimbali kama vile majadiliano ya utekelezaji wa mradi huu katika eneo la Hifadhi ya Taifa ya Nyerere, mradi ulichelewa kuanza utekelezaji wake kwa takribani miezi 17.

Aidha, uwepo wa ugonjwa wa Covid – 19 umechangia kwa kiasi kikubwa kuendelea kuchelewesha utekelezaji wa mradi huu. Kutokana na kazi nyingi kusimama, mradi huu sasa umeshaanza kutekelezwa.

Mheshimiwa Spika, ili kukabiliana na changamoto zote ambazo zilijitokeza, mradi umefanyiwa mapitio ya kati ambapo miongoni mwa mambo mengine ni kuongeza muda wa utekelezaji wa mradi huu hadi mwaka 2025 ili kufidia muda uliopotea.
Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha.