Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 11 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 84 2021-04-16

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. CHARLES M. KAJEGE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itazikarabati barabara za Jimbo la Mwibara ambazo zimeharibika sana ili kuruhusu mawasiliano kwa wananchi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Charles Mugeta Kajege, Mbunge wa Jimbo la Mwibara kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ina majimbo mawili ya Uchaguzi ambayo ni Bunda Vijijiini na Mwibara yenye mtandao wa barabara wenye urefu wa kilomita 527.55. Serikali imekuwa ikitenga fedha za matengenezo ya barabara katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda ambapo katika mwaka wa fedha 2019/20 shilingi milioni 546.87 zilitumika kwa ajili ya matengenezo ya barabara na shilingi bilioni 708.56 zimeidhinishwa katika mwaka wa fedha 2020/21 kwa ajili ya matengenezo ya barabara katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Mheshimiwa Spika, ili kuboresha miundombinu ya barabara katika jimbo la Mwibara katika mwaka wa fedha 2019/2020 Serikali imefanya matengenezo ya barabara zenye urefu wa kilomita 28.2 na makalvati 11 kwa gharama ya shilingi milioni 237. 43. Aidha, katika mwaka wa fedha 2020/ 21 shilingi milioni 460.44 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara zenye urefu kilomita 54.5 na makalvati 29 ambapo utekelezaji unaendelea.

Mheshimwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha za ujenzi na matengenezo ya barabara za Wilaya ya Bunda na nchini kote kadri ya upatikanaji wa fedha.