Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 10 Water and Irrigation Wizara ya Maji 83 2021-04-15

Name

Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI K.n.y. MHE. ZAINAB A. KATIMBA aliuliza:-

Kijiographia Tanzania ipo kwenye ukanda wenye mvua za kutosha:-

Je, Serikali imejizatiti vipi kuhamasisha zoezi la uvunaji wa maji ya mvua kwa matumizi ya wananchi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zainabu Athman Katimba, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Nchi yetu ipo kwenye ukanda wa mvua za kutosha, hivyo ujenzi wa miundombinu ya kuvuna maji ya mvua ni muhimu kwa kuwa itawezesha kuwa na maji ya uhakika kwa kipindi chote cha mwaka bila kujali hali ya hewa. Vilevile, miundombinu hiyo ni muhimu kwa kuwa itawezesha kudhibiti mafuriko na pia kuokoa miundombinu, ikiwemo ya kuhudumia maji pamoja na mali na maisha ya wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutimiza azma hiyo mkakati mwingine ni Wizara ya Maji kukutana na TAMISEMI kwa lengo la kuhusisha mashule, kujenga gats za maji na matenki, pia kuhamasisha wananchi wanapojenga nyumba zao waweke miundombinu rafiki ya kukusanya maji, lengo zoezi liwe shirikishi. Aidha, Serikali inaendelea na mpango wa ujenzi wa ukarabati wa mabwawa kwa kila wilaya, hususan katika wilaya kame.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Mwaka wa Fedha 2020/21 Wizara imekamilisha ukarabati wa mabwawa ya Mwadila lililoko Wilaya ya Maswa Mkoa wa Simiyu, usanifu kwa ajili ya kukarabati mabwawa matatu ya Itobo lililoko Wilaya ya Nzega, Ingekument lililoko Wilaya ya Monduli na Horohoro lililoko Wilaya ya Mkinga na usanifu kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa mawili ya Muko na Chiwanda yaliyoko Wilaya ya Momba.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile, usanifu wa Malambo ya kunyweshea mifugo sita, umekamilika katika mwambao wa barabara kuu ya Dodoma Babati, ikihusisha Wilaya ya Bahi malambo mawili na Chemba malambo manne. Vile vile, Serikali inaendelea na mpango wa kujenga mabwawa ya kimkakati ya Kidunda Mto Ruvu, Falkwa katika Mto Bubu na Ndembela Lugoda katika Mto Ndembela.