Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 9 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 74 2021-04-14

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUDITH S. KAPINGA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutenganisha fedha za maendeleo ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Fedha za Bodi ya Mikopo kwa kuzitengea Vote tofauti fedha hizi za mikopo ili kuleta tija ya miradi ya maendeleo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia naomba kujibu swali la Mheshimiwa Judith Salvio Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ndiyo yenye dhamana ya kuendeleza mtaji watu kwa ajili ya mipango na maendeleo ya Taifa letu. Aidha, lengo la mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu, ni kuongeza mtaji watu katika nchi yetu. Hivyo, utengaji wa fedha za mikopo ya elimu ya juu chini ya Fungu 46, ulizingatia majukumu ya Fungu husika ambayo ni kuandaa na kuendeleza mtaji watu kwa ajili ya maendeleo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuongeza rasilimali fedha katika Sekta ya Elimu kwa lengo la kukabiliana na changamoto zilizopo. Hivyo, Serikali itaendelea kutafuta fedha zaidi ili kuendeleza hatua zake za kutatua changamoto zilizopo. Ahsante.