Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 49 2021-04-12

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga vituo vya afya katika Kata za Tinginya, Muhimba, Kalulu, Mindu, Nalasi Magharibi na Nalasi Mashariki Wilayani Tunduru?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jacqueline Ngonyani Msongozi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha huduma za afya katika ngazi zote nchini ikiwemo Wilaya ya Tunduru. Katika kipindi cha kuanzia mwaka 2017 hadi 2020 Serikali imejenga na kukarabati Vituo vinne (4) vya Afya vya Mkasale, Matemanga, Mchoteka na Nakapanya Wilayani Tunduru kwa gharama ya shilingi biloni 1.5. Aidha, katika Mwaka wa Fedha 2020/2021 Serikali imetenga shilingi milioni 200 kwa ajili ya kukamilisha maboma manne (4) ya zahanati katika Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kwamba mahitaji ya vituo vya kutolea huduma za afya ni mengi nchini, ikiwemo Wilaya ya Tunduru. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga na kukarabati vituo vya kutolea huduma za afya nchini ikiwemo vituo vya afya kwenye Kata za Tinginya, Muhimba, Kalulu, Nalasi Magharibi na Nalasi Mashariki katika Wilaya ya Tunduru kwa kadri ya upatikanaji wa fedha.