Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 44 2021-04-09

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza:-

Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete ya ujenzi wa bwawa la maji katika Kata ya Mikangaula Wilayani Nanyumbu itatekelezwa?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahya Ally Mhata, Mbunge wa Nanyumbu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Serikali iliahidi kuboresha huduma ya maji katika Wilaya ya Nanyumbu kwa kujenga mabwawa katika Vijiji vya Mikangaula, Mchiga, Maratani, Chilunda na Nangova.

Katika kutekeleza ahadi hiyo, Serikali imeanza ujenzi wa bwawa katika Kijiji cha Maratani ambapo ujenzi wake umefikia asilimia 95 na utakamilika mwishoni mwa mwezi Aprili, 2021. Kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa tuta, spill-way, chemba za kutolea maji na kupokea maji, birika la kunyweshea mifugo na kituo kimoja cha kuchotea maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mwaka wa fedha 2021/ 2022, RUWASA Wilaya ya Nanyumbu imepanga kuanza kazi za ujenzi wa mabwawa ya Mikangaula na Chilunda.