Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 4 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 51 2021-09-03

Name

Shanif Mansoor Jamal

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwimba

Primary Question

MHE. KASALALI E. MAGENI K.n.y. MHE. SHANIF M. JAMAL Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Hungumalwa - Ngudu hadi Magu kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) Alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Shanif Mansoor Jamal, Mbunge wa Kwimba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya kutoka Hungumalwa – Ngudu hadi Magu ni barabara ya Mkoa yenye urefu wa kilometa 71. Barabara hii ni kiunganishi muhimu kati ya Wilaya za Kwimba na Magu kupitia Hungumalwa - Ngudu - Bukwimba hadi Isandula Wilayani Magu.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara (TANROADS) ilikamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Hungumalwa – Ngudu – Bukwimba – Magu yenye urefu wa kilometa 71 mwaka 2019. Katika mwaka huu wa fedha wa 2021/2022 Serikali imetenga shilingi milioni 1,500 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami, Serikali kupitia (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka ambapo katika mwaka huu wa fedha jumla ya shilingi milioni 926.711 zimetengwa. Ahsante. (Makofi)