Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 3 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 38 2021-09-02

Name

Omar Ali Omar

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Wete

Primary Question

MHE. OMAR ALI OMAR Aliuliza:-

Je ni lini Serikali itatoa ajira kwa Jeshi la Polisi, hasa ikizingatiwa kuwa haijatoa ajira tangu mwaka 2015?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu: -


Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimwa Omar Ali Omar, Mbunge wa Jimbo la Wete kutoka Mkoa wa Kaskazini Pemba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kuajiri na kuongeza idadi ya askari polisi hapa nchini kwani idadi yao hupungua kutokana na askari kustaafu, kufariki dunia, kufukuzwa kazi na wengine kuacha kazi, napenda kumtaarifu Mheshimiwa Mbunge kuwa Serikali kupitia bajeti yake ya mwaka 2021/2022 imetoa kibali cha ajira kwa askari polisi 3,103 ambapo mchakato wake unaendelea hivi sasa. Nakushukuru.