Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Madini 26 2021-09-01

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatoa matokeo ya tafiti za madini katika lugha nyepesi kwa wachimbaji wadogo ili ziwasaidie katika uchimbaji kwa kuwa Sheria ya Madini inazitaka Kampuni zinazofanya utafiti kwenye madini kuwasilisha matokeo ya tafiti hizo GST?

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Masache Njelu Kasaka, Mbunge wa Jimbo la Lupa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) tangu mwaka 2019 imekuwa ikitoa matokeo ya tafiti za madini kwa lugha ya Kiswahili na iliyorahisishwa ili kuwawezesha wachimbaji wadogo kuelewa kwa urahisi. Aidha, GST imeandaa kitabu mahususi chenye Kichwa “Kitabu cha Madini Yapatikanayo Tanzania” ambacho nacho kimeandaliwa kwa lugha ya Kiswahili na kinabainisha maeneo yenye viashiria vya madini ya aina mbalimbali yanayopatikana nchini.

Mheshimiwa Spika, sambamba na hilo, GST imeandaa Kitabu cha Mwongozo wa Uchukuaji wa sampuli za madini na kitabu hicho ni cha mwaka huu huu wa 2021 ambacho pia kimeandaliwa kwa lugha fasaha ya Kiswahili, nyepesi na inayoeleweka, lengo likiwa ni wachimbaji wetu wadogo waweze kufaidika na lugha hiyo iliyorahisishwa. Ahsante.