Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 25 2021-09-01

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA Aliuliza:-

(a) Je, ni lini mahabusu wataruhusiwa kushiriki katika shughuli za uzalishaji mali wakiwa Gerezani?

(b) Je, ni nini kauli ya Serikali katika kuwezesha Magereza kwa chakula kwa kuwa mkakati wa kila Gereza kujitegemea kwa chakula umeshindwa kutekelezeka?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Neema Gerald Mwandabila, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Songwe, kama ifuatavyo:-

(a) Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kifungu cha 78(1) cha Sheria ya Magereza, Sura 58 iliyorejewa Mwaka 2002, kimeeleza kuwa, pamoja na mahabusu kulazimika kufanya kazi za usafi kwenye bweni analoishi na usafi wa mwili wake, vyombo anavyotumia, nguo na samani anazotumia, pia anaweza kufanya kazi za uzalishaji kwa ridhaa yake. Kifungu hiki kinasomwa sambamba na Kanuni Na. 421 ya Kanuni za Kudumu za Magereza, Toleo la Nne la Mwaka 2003.

(b) Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mpango wa kujitosheleza kwa chakula Magerezani umeanza kwa magereza nane (8) ya Songwe, Kitai, Kitengule, Mollo, Pawaga, Arusha, Ushora na Ubena kwa lengo la kuzalisha kwa wingi na kusambaza chakula katika magereza mengine ambayo hayapo kwenye mpango. Uwezo wa kujitosheleza kwa chakula cha wafungwa umeongezeka na kufikia 54% kwa mwaka 2020/2021 ikilinganishwa na 23% kwa mwaka 2019/2020.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/2022 Serikali imetenga shilingi bilioni sita kwa ajili ya kuongeza mashamba na kuimarisha miundombinu na zana za kilimo ili kuongeza uzalishaji na kuyafikia malengo ya kujitosheleza kwa chakula.