Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 1 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 11 2021-08-31

Name

Mohammed Maulid Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Primary Question

MHE. MOHAMMED MAULID ALI Aliuliza:-

(a) Je, Serikali inatambua mgogoro wa ardhi baina ya wananchi na Kambi ya Jeshi la Wananchi iliyopo Chukwani Zanzibar?

(b) Je, Waziri yupo tayari kufuatana na Mbunge ili kukutana na wananchi na kufahamu hali halisi ya mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI K.n.y. WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maulid Ali Mohammed, Mbunge wa Jimbo la Kiembe Samaki lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-


(a) Mheshimiwa Spika, Kambi ya Chukwani imepimwa na inatambuliwa kama Kiwanja Namba 787 na ramani yake imepata usajili Namba S.40/07. Eneo hili limepewa Hati Miliki Namba Z.20.2007. Hata hivyo, kuna wananchi wachache wanafanya shughuli za kibinadamu ndani ya eneo la kambi. Wananchi hawa sio wavamizi, wanatakiwa kulipwa fidia kwani ni maeneo yao ya siku nyingi kabla ya Jeshi kutwaa na kupima eneo hilo, pia ilikubalika waondoke baada ya kufanyiwa uthamini na kulipwa fidia.

Mheshimiwa Spika, Wizara inatambua mgogoro huo na hivi sasa ipo katika mpango wa miaka mitatu wa kuondoa migogoro yote iliyopo katika maeneo yake ikiwemo Kambi ya Jeshi ya Chukwani iliyopo Zanzibar. Mpango huo utajumuisha na kupatiwa Hati Miliki za maeneo yake yote.

(b) Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa alikuwa anauliza kwamba tupo tayari kwenda kuonana na wananchi. Nimwambie tu kwamba tupo tayari kwenda kuonana na wananchi ili tuweze kukaa nao, tujue sasa asili na chanzo cha mgogoro huo na tuwaeleze hatua ambayo tumefikia kama Serikali. Nakushukuru.