Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 9 2021-08-31

Name

Saada Mansour Hussein

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAADA MONSOUR HUSSEIN Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawapatia Vitambulisho vya NIDA wananchi wote waliojiandikisha?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Saada Monsour Hussein, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kaskazini Unguja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Mpango wa Serikali ni kuhakikisha watu wote waliosajiliwa na kupata namba za utambulisho wanazalishiwa na kugawiwa vitambulisho vya Taifa.

Mheshimiwa Spika, hadi kufikia mwezi Agosti, 2021, Serikali kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) imefanikiwa kuzalisha na kugawa kwa wananchi jumla ya vitambulisho 8,397,524. Aidha, Mamlaka inaendelea na mpango kazi wa uzalishaji ambapo wananchi wote wenye sifa watazalishiwa na kugawiwa vitambulisho vyao ifikapo tarehe 31 Desemba, 2021. Nakushukuru.