Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 42 2021-04-09

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO Aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza transfoma ya 100 MVA katika substation ya Mbagala ili kuondoa tatizo la kukatika umeme katika Jimbo la Mbagala?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Jafari Chaurembo, Mbunge Wa Mbagala, kama Ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa kituo cha kupoza umeme cha Mbagala msongo wa kilovoti 132/33 chenye uwezo wa MVA 50 ulikamilika na kuanza kufanya kazi rasmi tarehe 25 Februari 2018, kupitia utekelezaji wa mradi wa TEDAP chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia. Baada ya kituo hiki kuanza kufanya kazi, hali ya upatikanaji umeme katika eneo la Mbagala uliimarika ikilinganishwa na kipindi cha nyuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kukamilika kwa ujenzi wa kituo hicho cha kupoza umeme, Serikali kupitia TANESCO inatekeleza mradi wa kuboresha vituo vya kupoza umeme vya Kinyerezi na Mbagala kwa kufunga transfoma zenye uwezo wa MVA 50 kwa kila kituo pamoja na kuongeza uwezo wa njia ya kusafirisha umeme ya kilovoti 132 kutoka Kinyerezi hadi Mbagala kupitia Gongo la Mboto. Mradi huu unatarajia kutekelezwa kwa kipindi cha miezi kumi kuanzia Juni, 2021 na kukamilika Aprili, 2022. Gharama ya mradi huu ni takriban Dola za Marekani milioni 9.

Mheshimiwa Naibu Spika, kukamilika kwa utekelezaji wa mradi huu, kutaboresha hali ya upatikanaji umeme katika maeneo ya Mbagala na maeneo mengine ya jirani yanayopatiwa umeme kutoka katika kituo hicho.