Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 41 2021-04-09

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KUNTI Y. MAJALA Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itasambaza umeme katika Kata za Handa, Lalta, Sanzawa na Mpendo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kunti Yussuf Majala, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji ambavyo havijapata umeme katika Wilaya ya Chemba vikiwemo vijiji vya Kata za Handa, Lalta, Sanzawa na Mpendo vitapatiwa umeme kupitia mradi wa REA awamu ya tatu mzunguko wa pili ulioanza kutekelezwa mwezi Machi, 2021 na utekelezaji wa mradi huu utakamilika ifikapo Desemba, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, kazi za mradi kwa Wilaya ya Chemba zinajumuisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 umbali wa kilomita 681.4, msongo wa kilovoti 0.4 umbali wa kilomita 50, ufungaji wa transfoma 50 za 50kVA, pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali wapatao 1,100 kwa gharama ya takriban Shilingi Bilioni 27.3.