Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 2 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 20 2021-03-31

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa amana na hisa za wateja waliokuwa wamewekeza katika Benki ya Wananchi Meru ambayo ilifungiwa kutoa huduma za kibenki Mwaka 2018?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO Alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Dkt. John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, mnamo tarehe 4 Januari, 2018 Benki Kuu ya Tanzania iliifutia leseni Benki ya Wananchi wa Meru kutofanya biashara za kibenki kwa mujibu wa vifungu Na. 11(3)(1), 41(a), 58(2) na 61(1) ya Sheria ya mabenki na taasisi ya fedha ya mwaka 2006.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kufuatia leseni benki hizo Benki Kuu ya Tanzania iliiteua Bodi ya Bima ya Amana kwa ufilisi. Katika kutimiza wajibu wake wa msingi kisheria, Bodi ya Bima ya Amana ilianza zoezi la kulipia fidia ya kulipia fidia ya bima ya amana hadi shilingi 1,500,000 kwa wateja waliostahili kulipwa bima ya amana, na zoezi hilo bado linaendelea kwa wateja ambao hawajajitokeza kuchukua fidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia mwisho wa mwezi wa Februari, 2021 jumla ya shilingi bilioni 1.47 zimeshilipwa kwa wateja waliokuwa na amana katika benki hiyo. Malipo hayo ambayo ni sawa na asilimia 78.70 ya kiasi cha shilingi bilioni 1.86 zilizotengwa kwa ajili kulipia fidia. Aidha, jumla ya wateja waliolipwa 4,679 kati ya wateja 13,138, ikiwa ni asilimia 35.61 ya wateja waliokuwa na amana zinazostahili fidia.

Mheshimiwa Naibu Spika, wateja waliokuwa na amana inayozidi shilingi 1,500,000 watalipwa kiasi kilichobaki chini zoezi la ufilisi, ambapo kwa mujibu sheria na taratibu za ufilisi kiasi kitakacholipwa kitategemea fedha zitakazopatika kutokana na kuuza mali za benki husika. Zoezi hili la kukusanya madeni na mali za Benki ya Wananchi Meru ili kupata fedha ya kuwapatia wateja wenye amana zenye thamani ya shilingi 1,500,000 pamoja na wanahisa wa benki hii bado linaendelea. Ahsante.