Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 11 2021-03-31

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. NAPE M. NNAUYE K.n.y. MHE. HASSAN S. MTENGA Aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza ruzuku katika mpango wa utoaji bure Elimu ya Sekondari na Msingi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Seleman Mtenga, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kutekeleza Mpango wa Elimumsingi Bila Malipo nchini ulioanza kutekelezwa mwezi Desemba, 2015. Fedha zinazotolewa kupitia mpango huo zinahusisha fidia ya ada, shughuli za uendeshaji wa shule, fedha za chakula kwa shule za bweni na malipo ya posho za madaraka kwa Wakuu wa Shule na Maafisa Elimu Kata.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali inaomba kutengewa kiasi cha shilingi bilioni
312.09 kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango wa Elimu Bila Malipo ambalo ni ongezeko la shilingi bilioni 13.96 ikilinganishwa na shilingi bilioni 298.13 zilizoidhinishwa katika mwaka wa fedha 2020/2021. Serikali itaendelea kutenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mpango wa Elimumsingi Bila Malipo kwa kadiri ya mahitaji na upatikanaji wa fedha. Aidha, kuanzia mwezi Desemba, 2015 hadi Februari mwaka 2021, Serikali imetoa kiasi cha shilingi trilioni 1.26 kwa ajili ya Elimumsingi Bila Malipo.