Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 1 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 9 2021-03-30

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Primary Question

MHE. JUMANNE A. SAGINI Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itazipatia umeme kaya na vitongoji ambavyo havijapatiwa umeme Wilayani Butiama?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jumanne Abdallah Sagini, Mbunge wa Butiama, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa kupeleka umeme katika mitaa na vitongoji ambavyo havijapata umeme ikiwemo Wilaya ya Butiama. Serikali imeanza maandalizi ya kutekeleza mradi unaohusishwa ujenzi wa miundombinu ya umeme ya njia ya msongo wa kilovoti 0.4 zenye urefu wa kilometa 1,620, ufungwaji transforma 648 na kuunganisha wateja wa awali 48,600 katika vitongoji 648 nchini ikiwa ni pamoja na kaya na vitongoji vya Wilaya ya Butiama ambavyo havijapata umeme. Gharama ya mradi huuni shilingi bilioni 75. Ujenzi wa mradi huu unatarajiwa kuanza julai, 2021 na kukamilika mwezi Desemba, 2022.

Mheshimiwa Naibu Spika, kukamilika kwa utekelezaji wa mradi huu kutatimiza azma ya Serikali ya kufikisha huduma ya umeme katika vitongoji vyote vya Wilaya ya Butiama.