Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 1 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 2 2021-03-30

Name

Najma Murtaza Giga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAJMA MURTAZA GIGA Aliuliza:-

(a) Je, Serikali inasemaje kuhusiana na ongezeko la vitendo vya ubakaji na udhalilishaji wa watoto nchini?

(b) Je, kwa nini Serikali haifanyi tafiti kujua sababu za kesi nyingi kushindwa kuwatia hatiani wabakaji na kuja na mpango mpya wa kudhibiti vitendo hivyo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi naomba kujibu maswali ya Mheshimiwa Najma Murtaza Giga, Mbunge wa Viti Maalum yote mawili kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ni wajibu wa Serikali kuwalinda wananchi wakiwemo watoto dhidi ya makosa ya ubakaji na udhalilishaji. Ili kupambana na vitendo hivi Serikali imekuwa ikichukua hatua kali ikiwemo kifungo cha miaka 30 jela kwa wanaojihusisha au kusaidia kufanyika kwa vitendo hivi.

Mheshimiwa Naibu Spika, tafiti nyingi zimefanywa na asasi mbalimbali za Serikali na zisizokuwa za Kiserikali na zimebaini kwamba kuna sababu mbalimbali ambazo zinasababisha. Sababu hizi zikiwemo sababu za muhali lakini pia kuna sababu za kumalizana nje ya Mahakam ana wahanga kuchelewa kuripoti vituo vya polisi. Kwa kipindi cha mwaka 2020 jumla ya washtakiwa 1,183 walihukumiwa vifungo jela.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia Bunge lako tukufu naomba kutoa wito kwa Waheshimiwa Wabunge na wananchi kwa ujumla kutoyafumbia macho matukio ya udhaliliishaji na ubakaji ikiwemo kutoa taarifa kwa vyombo vya dola vinavyohusika. Ahsante.