Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 9 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 125 2021-02-12

Name

Florent Laurent Kyombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkenge

Primary Question

MHE. FLORENT L. KYOMBO Aliuliza:-

Pamoja na kazi nzuri ya miradi ya kutengeneza barabara Nkenge, viongozi wetu kwa nyakati tofauti wameahidi kufanya maboresho ya miundombinu ya barabara za Kabyaile/Shozi – Njiapanda ya Gera, Minziro – Mutukula, Kaja Hospitali ya Mugana (Bwanja).

Je, ni lini barabara hizo zitatengenezwa ili kuondokana na kero hizo zinazowapata wananchi wanaotumia barabara hizo kiuchumi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Florent Laurent Kyombo, Mbunge wa Nkenge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Mutukula – Minziro (kilometa 15.8) ni barabara ya ulinzi na pia ni moja ya ahadi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Barabara hiyo inatakiwa kufunguliwa na tayari kilometa mbili zipo na zinatumika. Kilometa 13.8 zilizosalia zinapita katika mashamba na Hifadhi ya Msitu wa Minziro na zitaendelea kufunguliwa kwa awamu. Makisio ya ujenzi wa barabara hiyo yamefanyika na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS)ambapo jumla ya shilingi bilioni 3.63 zinahitajika kwa ujenzi wa kiwango cha changarawe na shilingi bilioni 9.994 zinahitajika kwa ujenzi wa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara zingine ambazo Mheshimiwa Mbunge amezitaja, Serikali itaendelea kuziboresha ili kuhakikisha kuwa zinapitika vizuri katika majira yote ya mwaka. Ahsante.