Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Madini 107 2021-02-11

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA Aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti ili kubaini uwepo wa aina mbalimbali za madini katika Jimbo la Manyoni Mashariki hususan Kata za Sasilo, Makuru, Kintinku na Solya?

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Taasisi yetu ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (Geological Survey of Tanzania - GST) kwa nyakati tofauti imefanya utafiti wa awali, nisisitize tu utafiti wa awali katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania zikiwemo Kata za Makuru, Solya, Kintinku na Sasilo ambako ndiko Mheshimiwa Mbunge anatoka.

Mheshimiwa Spika, matokeo ya tafiti za awali zilizofanyika katika maeneo hayo zinaonesha kuwa kuna viashiria vya uwepo wa madini kama ifuatavyo:-

(a) Katika Kata ya Makuru – kuna dhahabu kidogo pamoja na ulanga (nickel);

(b) Katika Kata ya Solya – Kuna urani, thorium na madini ya ujenzi;

(c) Katika Kata ya Kintinku – kuna Urani; na

(d) Katika Kata ya Sasilo – kwa utafiti uliofanyika hakukuonekana kwamba kuna viashiria vya uwepo wa madini.

Mheshimiwa Spika, ili kuwezesha uchimbaji kufanyika, mara nyingi sana tafiti za kina zinahitajika ili kujiridhisha na kiwango cha mashapo iwapo yanaweza kuchimbwa kwa faida au la.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.