Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 8 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 105 2021-02-11

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. ABUBAKAR D. ASENGA Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaongeza uwekezaji wa Kiwanda cha Sukari Kilombero ili kunusuru miwa ambayo haijavunwa kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abubakari Damian Asenga, Mbunge wa Kilombero, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaona kuna umuhimu wa kuongeza uzalishaji wa sukari nchini ili kukabiliana na changamoto ya uhaba wa sukari ambao umekuwa ukijitokeza mara kwa mara. Kwa msingi huo, hoja ya kuongeza uwekezaji katika Kiwanda cha Sukari cha Kilombero ni ya msingi sana.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina imekuwa ikisimamia utendaji kazi wa Kiwanda hiki cha Sukari cha Kilombero kwa ukaribu kama inavyosimamia kampuni nyingine ambazo Serikali ina hisa chache kwa mujibu wa Sheria ya Msajili wa Hazina, Sura 370. Serikali pamoja na Mbia Mwenza (Kilombero Holding Limited) imekuwa kwenye majadiliano ya kina kuhusu kuongeza uzalishaji wa kiwanda hiki kwa kufanya upanuzi wa kiwanda ambapo imekubaliana kupitia gharama za upanuzi wa kiwanda, kufanya upembuzi yakinifu na namna ya ugharamiaji wa mradi. Mara baada ya zoezi hili kukamilika uwekezaji katika kiwanda hiki utafanyika haraka iwezekanavyo. (Makofi)