Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 6 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 82 2021-02-09

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kiwango cha lami wa barabara ya Lupiro – Malinyi – Londo – Namtumbo, yenye urefu wa kilometa 296 ambayo ipo katika Ilani ya CCM 2020?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Lupiro – Malinyi – Londo – Namtumbo yenye urefu wa kilometa 296 ni sehemu ya barabara kuu ya Mikumi – Kidatu – Ifakara – Malinyi – Kilosa kwa Mpepo – Londo – Lumecha yenye kilometa 547 ambayo inaunganisha Mikoa ya Morogoro na Ruvuma.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kwa kuzingatia umuhimu wa barabara hii, Wizara kupitia TANRAODS, imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina mwaka 2018. Ujenzi wa sehemu ya Kidatu – Ifakara kilometa
66.9 kwa kiwango cha lami pamoja na Daraja la Ruaha Mkuu unaendelea. Fedha kwa ajili ya ujenzi wa sehemu iliyobaki ikiwemo ya Lupiro – Malinyi – Londo – Namtumbo zinaendelea kutafutwa na Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati ikiendelea kutafuta fedha za ujenzi, Serikali pia imeendelea kutenga fedha za matengenezo mbalimbali ya barabara hii, ambapo katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya shilingi milioni 720 na shilingi milioni 377.2 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya barabara hii katika mikoa ya Morogoro na Ruvuma mtawalia ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Ahsante.