Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 5 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 67 2021-02-08

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY Aliuliza: -

Je, lini Serikali itaongeza bajeti ya kuboresha elimu katika Vyuo vya Ufundi (VETA) Mkoani Manyara ili kuboresha utoaji wa elimu ya ufundi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Regina Ndege Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiongeza wigo wa bajeti kwa ajili ya kutekeleza mipango mbalimbali ya kuboresha utoaji wa elimu na mafunzo ya ufundi nchini. Mkoa wa Manyara ni moja kati ya mikoa inayonufaika na ongezeko hilo la bajeti. Katika kipindi cha mwaka 2018 – 2020, Serikali imetumia kiasi cha shilingi 1,925,438,420.13; kati ya fedha hizo shilingi 600,000,000 zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu na shilingi 505,159,420.00 zimetumika kununua nyumba za watumishi katika chuo cha VETA Manyara kutoka Shirika la Nyumba la Taifa.

Mheshimiwa Spika, katika Chuo cha VETA Gorowa, kiasi cha shilingi 337,081,677.13 kimetumika kwa ajili ya ujenzi wa karakana, ofisi ya utawala na madarasa. Vilevile, katika Chuo cha VETA Simanjiro Serikali imetumia kiasi cha shilingi 223,981,323.00 kwa ajili ya kununulia vifaa vya kufundishia na kujifunzia na kujenga bweni la wasichana. Aidha, shilingi 259,279,000.00 zimetumika kugharamia mafunzo ya muda mfupi katika Vyuo vya VETA Manyara na Gorowa.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuongeza bajeti kwa ajili ya kuboresha utoaji wa elimu na mafunzo ya ufundi katika mkoa wa Manyara na mikoa mingine kwa ujumla kulingana na upatikanaji wa fedha.