Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 17 Finance and Planning Ofisi ya Rais TAMISEMI. 143 2016-05-11

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Primary Question

MHE. CONSTANTINE J. KANYASU aliuliza:-
Shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu ilijengwa na mradi wa GGM kusaidia kundi kubwa la wasichana wasome Wilayani Geita, shule hii ina hosteli za kutosha na nyumba za walimu.
Je, ni kwa nini shule hiyo imebaki kuwa shule ya kutwa wakati mazingira yake yanafaa kuwa sekondari ya bweni?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kanyasu Constantine John, Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shule ya Wasichana Nyankumbu ilijengwa chini ya mradi wa Geita Gold Mining na kupata usajili Na. S. 1942 mwaka 2006 ikiwa ni shule ya kutwa kwa kidato cha kwanza hadi cha nne. Aidha, mwaka 2012 iliongezewa kidato cha tano na sita. Hivyo shule hiyo imesajiliwa kuwa ya kutwa kwa kidato cha kwanza hadi cha nne na bweni kwa kidato cha tano na sita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, taratibu zinazotumika ili kuisajili shule kuwa ya bweni, ni Halmashauri yenyewe kupeleka maombi Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi ili kupata kibali.
Aidha, kabla ya kupata usajili huo, Kamishna wa Elimu atatuma timu ya wataalam katika shule husika kwa ajili ya kuhakiki uwepo wa miundombinu inayohitajika ili shule iweze kusajiliwa kuwa ya bweni.