Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 54 2021-02-05

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO Aliuliza:-

Ofisi ya TANESCO Wilaya ya Muleba inazidiwa na wingi wa wateja kutokana na miradi ya REA.

Je, ni lini Wilaya hiyo itapewa hadhi ya Mkoa wa TANESCO ili iweze kutoa huduma kwa wakati?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Oscar Ishengoma Kikoyo, Mbunge wa Muleba Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Shirika la Umeme nchini (TANESCO) limekuwa likiweka ofisi za Mikoa katika maeneo mbalimbali kwa kuzingatia vigezo mbalimbali ikiwa ni pamoja na ongezeko la shughuli za kiutendaji za Shirika na mahitaji ya umeme pamoja na wateja.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kusogeza huduma kwa wateja karibu Wilayani Muleba, TANESCO imefungua ofisi ndogo (sub-office) eneo la Kamachumu na imeshaanza kutoa huduma kwa wateja wa Kamachumu katika Jimbo la Muleba Kaskazini na maeneo mengine ya jirani.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, TANESCO inatarajia kufungua ofisi ndogo (sub-office) nyingine eneo la Kyamyorwa na Bulyage ili kusogeza karibu zaidi huduma kwa wateja wa maeneo hayo na jirani. Ofisi hizo zitakuwa na wafanyakazi pamoja na vitendea kazi vyote vinavyohitajika ikiwa ni pamoja na usafiri.