Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2021-02-02

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA Aliuliza:-

Je, Serikali imefikia hatua gani katika utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Mwendokasi awamu ya tatu toka Gongolamboto mpaka Kariakoo ambao umeainishwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020 – 2025?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Ukonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Jijini Dar es Salaam (DART) inaendelea na utekelezaji wa mradi wa mabasi yaendeayo haraka maarufu kama mwendokasi unaotekelezwa katika awamu sita katika barabara zote kuu Jijini Dar es Salaam zenye urefu wa kilometa 146.2.

Mheshimiwa Spika, awamu ya tatu ya mradi wa mabasi yaendayo haraka inatekelezwa katika barabara za Nyerere, Bibi Titi, Maktaba, Azikiwe na Uhuru kutoka katikati ya Jiji la Dar es Salaam hadi Gongolamboto zenye urefu wa kilometa 23.6 ikiunganishwa na awamu ya kwanza na ya pili ya mradi huu katika vituo vikuu vya mabasi ya Kariakoo, Gerezani na Kivukoni.

Mheshimiwa Spika, kazi inayoendelea sasa ni tathmini ya zabuni zilizowasilishwa ili kumpata mkandarasi atakayeanza kujenga awamu ya kwanza ya mradi, kwa maana ya Lot 1, inayohusisha ujenzi wa barabara, kwa maana ya road works, vituo vidogo vya mabasi pamoja na kituo kikuu cha mabasi cha Gongolamboto.

Mheshimiwa Spika, zabuni ya kazi ya ujenzi awamu ya pili, inayojumuisha ujenzi wa karakana ya Gongolamboto, Kituo Kikuu cha Mabasi cha Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere pamoja na vituo mlisho vya Jet Club, Banana na Mombasa, zabuni yake haijatangazwa kutokana na mabadiliko ya usanifu wa karakana ya Gongolamboto baada ya eneo la karakana hiyo kubadilishwa kutokana na sehemu kubwa ya eneo la awali kuathiriwa na mradi wa reli ya kisasa.