Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 6 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 52 2020-04-08

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. JEROME D. BWANAUSI aliuliza:-

Serikali iliahidi kusambaza umeme katika Vijiji vya Matogolo na Nagaga.

(a) Je, ni lini vijiji hivyo vitasambaziwa umeme?

(b) Je, ni lini umeme jazilizi katika Jimbo la Lulindi utasambazwa?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jerome Dismas Bwanausi Mbunge wa Lulindi lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa kusambaza umeme vijiini katika vijiji vyote vya Tanzania Bara. Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwenzi Juni, 2021. Mradi wa REA III mzunguko wa kwanza unaoendelea utapeleka umeme katika vijiji 67 katika Wilaya ya Masasi kupitia Mkandarasi JV Radi Services Ltd., Njarita Contractors Ltd na Anguila Contractors Ltd.

Mheshimiwa Naibu Spika, Vijiji vya Matogolo na Nagaga vimeshapatiwa huduma ya umeme kupitia Shirika la Umeme nchini - TANESCO mwezi Februari, 2020. Kazi zinazoendelea kwa sasa ni maandalizi ya kusambaza umeme katika vitongoji vyote vya vijiji hivyo na kuunganishia umeme wateja.

Mheshimiwa Naibu Spika, Mradi wa Ujazilizi katika Jimbo la Lulindi Mkoani Mtwara utaanza kutekelezwa kupitia Mradi wa Ujazilizi Fungu la Pili (IIB) ambapo jumla ya Mikoa 16 itanufaika ikiwamo Mtwara. Miradi ya Ujazilizi IIB itawezesha kupeleka umeme katika vitongoji 2,400 na kuunganishiwa umeme wateja wa awali 95,000. Gharama na mradi ni Dola za Marekani milioni 100.

Mheshimiwa Naibu Spika, utekelezaji wa mradi huu utaanza mwezi Mei, 2020 na kukamilika ndani ya kipindi cha miezi 9.