Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 6 Water and Irrigation Wizara ya Maji 50 2020-04-08

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata za Kwai, Kilole, Kwekanga na Makanya katika Jimbo la Lushoto?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Jimbo la Lushoto kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kutatua tatizo la maji katika Wilaya ya Lushoto, Serikali tayari imekamilisha miradi ya Maji katika vijiji vya Mlalo/Mwangoi, Mlalo/Lwandai, Malibwi na Ngulu. Wananchi katika vijiji hivyo tayari wanapata huduma ya majisafi na salama na miradi mingine ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa, Kata ya Kwai kuna mradi wa maji unaotoa huduma katika Kijiji cha Kwai. Aidha, Kata ya Kwai na Makanya zipo kwenye mpango wa muda wa kati wa utekelezaji wa mradi mkubwa wa maji utakaotoa huduma ya maji katika vijiji 16 ambapo usanifu wake ulikamilika na kupata kibali cha utekelezaji. Mradi huo, umepangwa kutekelezwa katika mwaka ujao wa fedha wa 2020/2021.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu Kata ya Kilole, Kwekanga na Makanya Wizara imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni 57 kwa ajili ya kufufua visima vifupi vilivyopo ambavyo havifanyi kazi. Kazi hii itafanyika kupitia mpango wa malipo kwa matokeo (Payment by Results). Tayari vifaa vya ujenzi wa miradi hiyo vimenunuliwa na utekelezaji wa mradi unatarajiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Aprili 2020.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia umuhimu wa kuwaondolea adha ya upatikanaji wa maji wananchi, katika mwaka wa fedha 2019/2020, Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 1.18 kwa Halmashauri ya Lushoto ili kukamilisha miradi inayoendelea kutekelezwa katika vijiji vya Shume, Manolo, Madala, Gologolo, Ngwelo ambayo itahudumia jumla ya watu 48,781.