Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 19 | Sitting 6 | Health and Social Welfare | Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto | 46 | 2020-04-08 |
Name
Rose Cyprian Tweve
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:-
Serikali imekuwa ikihimiza wananchi kuchangia damu na kuihifadhi katika benki za damu kwa ajili ya watu wenye uhitaji.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanzisha utaratibu maalum wa kuvuna viungo kama vile figo na moyo kutoka kwa watu waliopata ajali na wapo kwenye hali ya kupoteza maisha au kutoka kwa watu walioridhia kutolewa viungo hivyo na kuvihifadhi kwa ajili ya Watanzania wenye uhitaji wa viungo hivyo?.
Name
Ummy Ally Mwalimu
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rose Cyprian Tweve Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ipo katika hatua za mwisho za kuandaa Muswada wa Sheria ya Uvunaji, Utunzaji, Usafirishaji na Upandikizaji wa viungo vya binadamu ikiwemo, Figo, Moyo, Maini, Mapafu, sclera ya macho, Uroto, IVF, pamoja na Stem cells itakayoweka utaratibu mzuri wa namna ya kufanya kazi hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria itaelekeza vitu vya kuzingatia kwa mpokeaji na mtoaji wa viungo. Sheria hii itaweka utaratibu kwa watu wanaoridhia kutolewa viungo vyao pindi wanapokaribia kupoteza maisha ikiwa mchangiaji (donor) huyo atakuwa ameridhia viungo vyake vitumike kwa ajili ya jamii inayohitaji viungo hivyo pindi akipoteza maisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, nchi yetu inaheshimu haki za binadamu ikiwemo haki ya kuishi, mtu kupata ajali na kutolewa viungo vyake litafanywa pale ambapo mhusika atakuwa ameridhia akipata ajali na akawa hana uwezo wa kupona atolewe viungo, basi hatua za kisheria na kitabibu zitatumika ili kutoa viungo hivyo na kuvihifadhi kwa ajili ya matumizi ya mtu atakayehitaji.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved