Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 19 | Sitting 5 | Justice and Constitutional Affairs | Katiba na Sheria | 43 | 2020-04-06 |
Name
Augustino Manyanda Masele
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbogwe
Primary Question
MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:-
Wananchi wa Wilaya ya Mbogwe wanapata changamoto kubwa katika kupata huduma za kimahakama kwa kuzifuata Wilaya za jirani:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Mahakama ya Wilaya Mbogwe?
Name
Dr. Augustine Philip Mahiga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Nominated
Answer
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, uhaba wa majengo ni moja ya changamoto inayoikabili Mahakama ya Tanzania. Mahitaji ya Majengo ya kuendeshea shughuli za Mahakama hapa nchini ni makubwa. Kwa msingi huo, Mahakama imejiwekea utaratibu wa kujenga majengo haya kwa awamu kulingana na mpango wa ujenzi na upatikanaji wa fedha.
Mheshimiwa Spika, ujenzi wa jengo la Mahakama ya Wilaya Mbogwe ni miongoni mwa Majengo ya Mahakama za Wilaya 33 yaliyopangwa kuanza kujengwa mwezi Juni na kukamilika mwezi Disemba, 2020 kwa ufadhili wa Benki ya Dunia. Kwa sasa Mahakama ipo katika hatua za mwisho kukamilisha taratibu za awali ili ujenzi wa majengo hayo uanze kwa muda kama ilivyo katika mpango wa Mahakama. Tayari Mshauri Elekezi amefanya mapitio ya michoro na ujenzi unatarajiwa kuanza kama ilivyopangwa.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved