Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 19 | Sitting 5 | Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives | Wizara ya Kilimo | 40 | 2020-04-06 |
Name
Anatropia Lwehikila Theonest
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:-
(a) Je, ni kwa nini Serikali inawazuia wakulima wanaoshirikiana na sekta binafsi, kuuza mazao yao ya biashara hasa kahawa, mahindi na korosho nje ya nchi kwa lengo la kujipatia faida?
(b) Je, ni kwa nini Serikali isiongeze ruzuku ya NFRA ili inunue mazao hayo pindi bei zinaposhuka?
Name
Japhet Ngailonga Hasunga
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Vwawa
Answer
WAZIRI WA KILIMO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anatropia Lweikila Theonest – Mbunge Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imekuwa na inaendelea kutoa vibali kwa wakulima na wafanyabiashara mbalimbali wanaosafirisha mazao ya kilimo hususan mahindi nje ya nchi au kuingiza ndani ya nchi. Vibali vitolewavyo na Wizara ya Kilimo ni vya kuingiza mazao ya kilimo nchini au kusafirisha mazao ya kilimo nje ya nchi (Import and Export Permits) pamoja na cheti cha Usafi wa Mazao yanayosafirishwa (Phytosanitary Certificate).
Mheshimiwa Spika, Serikali haina mpango wa aina yoyote wa kuwazuia wakulima kushirikiana na sekta binafsi kuuza mazao yao nje ya nchi na Serikali inaendelea kuhimiza wakulima waendelee kujiunga katika vikundi ili waweze kuwa na nguvu ya pamoja katika kuuza mazao yao na kuweza kuongezea thamani mazao yao ili waweze kujiongezea kipato zaidi.
(b) Mheshimiwa Spika, Majukumu ya Wakala wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (NFRA) ni kununua na kuweka akiba ya chakula cha Taifa, kudhibiti mfumuko wa bei wa vyakula vya nafaka kwa kuingiza nafaka sokoni ya bei nafuu pamoja na kutoa chakula cha msaada kwa maelekezo ya Mfuko wa Maafa wa Taifa pindi Taifa linapopatwa na majanga ya maafa. Kwa kuzingatia majukumu hayo, Wakala umekuwa kimbilio la wakulima kwa kuwa umekuwa ukinunua nafaka kwa bei nzuri katika masoko inayozingatia gharama za uzalishaji za mkulima.
Mheshimiwa Spika, Serikali hutenga ruzuku kwa ajili ya ununuzi wa nafaka kila mwaka. Kwa kuzingatia majukumu ya Wakala, ununuzi huu hauhusishi mazao yasiyo ya nafaka. Aidha, Wakala hutumia vyanzo vingine vya mapato kununua nafaka zikiwemo mauzo ya nafaka na mikopo kutoka taasisi za fedha, mikopo ambayo hurejeshwa kwa kutumia fedha za mauzo ya nafaka.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved