Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 39 2020-04-06

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. MARGARET S. SITTA aliuliza: -

Wilaya ya Urambo inakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji hadi Serikali ikaingiza Wilaya hii katika mpango mkubwa wa maji kutoka Ziwa Victoria, wakati wananchi wa Urambo wakisubiri mpango huo wa maji kutoka Ziwa Victoria:-

Je, ni lini Serikali itatimiza ahadi ya kuchimba visima 30 katika Wilaya ya Urambo?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Margareth Simwanza Sitta, Mbunge wa Urambo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kukabiliana na uhaba wa maji, Halmashauri ya Wilaya ya Urambo ilisaini Mkataba na uliokuwa Wakala wa Uchimbaji Visima (DDCA) tarehe 26 Machi, 2018 wa gharama ya Shilingi milioni 620.9 kwa ajili ya kuchimba visima 30 katika Vijiji vya Ussoke Mjini viwii; Itundu viwili; Kasisi viwili; Kiloleni viwili; Tulieni kimoja; Machinjioni kimoja; Ulassa B kimoja; Ifuta viwili; Ugalla viwili; Uyogo viwili; Nsenda viwili; Unzali viwili; Vumilia viwili; Kalembela viwili; Ussoke Mlimani viwili; Katunguru viwili; na Kapilula kimoja.

Mheshimiwa Spika, utafiti wa maeneo ya uchimbaji wa visima hivyo umekamilika na mradi huu utatekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) ambapo unatarajiwa kufanyika mwezi Mei, 2020.

Mheshimiwa Spika, vilevile, Wilaya ya Urambo kupitia Mpango wa Matokeo (PforR) imepanga kuchimba visima virefu 18 ili kupunguza tatizo la uhaba wa maji katika Vijiji vya Isongwa, Kichangani, Milambo, Ulassa A, Kamalendi, Mtakuja, Sipungu, Tumaini, Ukwanga, Itegamatwi, MotoMoto, Kalembela, Usoke Mlimani, Usoke Mjini, Itebulanda, Tebela, Kasisi na Vumilia. Utekelezaji wa kazi hiyo unatarajiwa kuanza mwezi Aprili, 2020.