Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2015-2020 | Session 19 | Sitting 5 | Works, Transport and Communication | Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano | 38 | 2020-04-06 |
Name
Issaay Zacharia Paulo
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Mbulu Mjini
Primary Question
MHE. ZACHARIA P. ISSAY aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mbulu mpaka Haydom kilometa 50 kama ilivyopitishwa kwenye bajeti ya 2019/2020?
Name
Eng. Isack Aloyce Kamwelwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Katavi
Answer
WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issay, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mbulu – Haydom kilometa 50 ni sehemu ya barabara ya Karatu, Mbulu, Haydom, Sibiti, Lalago – Maswa kilomita 389 ijulikanayo kama Serengeti Southern Bypass. Barabara hii inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) kupitia Mikoa ya Arusha, Manyara, Singida na Simiyu. Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali wa mradi wa Serengeti Southern Bypass iko katika hatua za mwisho. Mara baada ya upembuzi yakinifu na usanifu wa awali kukamilika hatua itakayofuata ni usanifu wa kina wa maandalizi ya nyaraka za zabuni kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mradi huu unahusisha barabara ndefu yenye urefu wa kilometa 389, ili kurahisisha utekelezaji wake wakati wa ujenzi, mradi huu umegawanywa katika sehemu saba ambazo ni Karatu – Mbulu kilometa 79; Mbulu - Haydom kilometa 70.5; Haydom - Chemichemi kilometa 67; Chemichemi - Mwanhuzi kilometa 80; Mwanhuzi – Lalago - Maswa kilometa 83; Haydom - Kadash kilometa 67 na Lalago - Kolandoto kilometa 62.
Mheshimiwa Spika, ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii utaanza baada ya kukamilisha usanifu wa kina.
Copyright © Bunge Polis 2021. All Rights Reserved