Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 4 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 29 2020-04-03

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO aliuliza:-

Mnamo tarehe 20 Mei, 2019 Kampuni ya Ultimate Security iliuzwa kwa asilimia mia moja kwa kampuni ya Garda World nchini Canada.

Je, Kampuni ya Garda World inatumia leseni ya kampuni ya ulinzi ya Ultimate Security au imeomba kubadili leseni ili isomeke kampuni mpya?

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Alhaji Abdallah Majura Bulembo, Mbunge wa Kuteuliwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa Kampuni ya Garda World ya Canada imeinunua Kampuni ya Ulinzi ya Ultimate Security. Aidha, kwa kuwa Garda World imeinunua Ultimate Security kwa asilimia mia moja na kwa kuwa kibali cha Ultimate Security bado kipo hai, Garda World wanaendelea kukitumia kwa mujibu wa taratibu na kanuni zinavyoelekeza.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa jina la Garda World linatumika kama chapa (brand) ya kibiashara tu na limesajiliwa BRELA kama taratibu zinavyoelekeza.