Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 4 Water and Irrigation Wizara ya Maji 28 2020-04-03

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza:-

Serikali ilishasema kwamba itatoa fedha ili maji yanayozalishwa na Mradi wa Maji BUWASA (Bukoba Water Supply and Sanitation Authority) yaweze kufika vijijini katika Kata za Maruku, Kanyangero, Kabaragaine, Katoma na Nyakato:-

Je, ni lini mradi huu utaanza kutekelezwa?

Name

Prof. Makame Mnyaa Mbarawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkoani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha wananchi wa Manispaa ya Mji wa Bukoba wanapata huduma ya majisafi na salama, mwaka 2016, Serikali ilikamilisha ujenzi wa mradi mkubwa wa maji. Aidha, baada ya kukamilisha mradi huo, Serikali imetoa fedha kwa ajili ya upanuzi wa mtandao wa maji ili wananchi wa maeneo ya Kata za Kibeta, Kagondo, Ijuganyundo na baadhi ya maeneo ya kata za Kahororo, Kashai, Nshambya na Nyaga waweze kunufaika kupitia mradi huo. Kwa sasa upanuzi huo umefikia asilimia 95. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kupeleka maji katika Kata za Maruku, Kanyangereko na Karabagaine.

Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Kata ya Katoma, Wizara kupitia Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imefanya usanifu ili kutumia Mto Kyeiringisa kama chanzo cha maji katika eneo hilo na Kata ya Nyakato itanufaika kupitia upanuzi wa awamu ya pili ya mtandao wa maji wa mradi mkubwa wa Manispaa ya Bukoba.