Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 19 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 27 2020-04-03

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:-

Mheshimiwa Rais amefanya marekebisho ya jina na mipaka ya iliyokuwa Halmashauri ya Wilaya ya Lindi na sasa kuna Halmashauri mpya ya Mtama inayojumuisha eneo lote la Jimbo la Mtama:-

Je, nini hatma ya eneo lililobaki la Jimbo la Mchinga ambalo hapo awali Lilikuwa ipo ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Lindi kama ilivyo kwa Jimbo la Mtama?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hamidu Hassan Bobali, Mbunge wa Mchinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kufuatia agizo la Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuhamishia Halmashauri ya Wilaya ya Lindi katika Jimbo la Mtama na Jimbo la Mchinga kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI inaendelea na uhakiki wa mipaka ili kundaa Tangazo la Serikali la kurekebisha mipaka ya Halmashauri hizo. Zoezi hilo linafanyika sambamba na maeneo mengine yaliyotangazwa na Mheshimiwa Rais ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.